Kuna Kila Dalili za Prof. Lipumba Kuwa Waziri wa Rais John Magufuli

Prof. Lipumba ni mmoja wa wamchumi nguli waliowahi kutokea nchini. Huyu bwana mbali tuu na kujivua uenyekiti wa chama chake cha CUF katika kipindi ambacho walikuwa wanamhitaji sana, lakini yeye amemkubali Rais JPM kuwa rais halali tofauti na msimamo wa chama chake ambacho kinaunda UKAWA.

Lakini hivi juzi alienda mbali mpaka kwenda Ikulu kumpongeza rais JPM. Kana kwamba haitoshi, mahakama imemfutia kesi yake na wafuasi wote alioshitakiwa nao kisa eti DPP kaamua kutoendelea na hiyo kesi. Hapo kuna maswali mengi ya kujiuliza???

Lakini vilevile Lipumba mara nyingi amekuwa na maoni chanya Kwa rais na CCM hali yeye mpinzani. Na yeye anajinasibu kuwa anapinga ufisadi na kitendo cha lowasa kwenda ukawa ni sawa na kumkaribisha fisadi.

Na JPM anasema hana ubia na mtu yeyote kwenye urais wake na kuna kila dalili za mawaziri kibao wa serikali iliyopita kupigwa chini kutokana na sifa ya utendaji mbaya. JPM haishiwi surprise na kutekeleza kile anachokiamini. Sasa je hizi si dalili za Prof Lipumba kuukwaa ubunge wa kuteuliwa na baadaye uwaziri wa serikali ya JPM???

Ni Mtizamo Wangu Tuu

Nafasi za Ajira


Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kwani bene?Aaa kumbe bene,,,,,,,,,

    ReplyDelete
  2. Bora maendeleo
    Kulikoni
    Kuchagua madomo kaya kina nape

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad