Mimba ya Jokate Aliyopewa na Mwimbaji Ali Kiba Yadaiwa Kuchoropoka

IMEFICHUKA! Ile mimba ya mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ iliyokuwa ikisemekana ni ya Mbongo-Fleva, Ali Saleh Kiba inadaiwa kuharibika kwa kuchoropoka kisa kikiwa ni mazoezi makali aliyoyafanya hivi karibuni.

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kwamba, Jokate kwa sasa hana ujauzito tena kwani ulichoropoka kufuatia mazoezi makali ya kujiandaa na shoo aliyofanya ya Nyama Choma Festival kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar iliyosapotiwa na mpenzi wake huyo.

Kama mlikuwa hamjui kitumbo cha Jojo (Jokate) kilichoropoka kutokana na mazoezi makali ya shoo aliyoifanya hivi karibuni ambapo kwa sasa anaendelea vizuri na anafanya kazi zake kama kawaida bila ujauzito,” kilinyetisha chanzo hicho.

Baada ya kupata habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Jokate na kumuuliza kuhusu ujauzito wake ambapo alijibu kwa ufupi: “Kwa sasa mimi sina mimba.”

Hata hivyo, chanzo hicho kiliendelea kueleza kwamba, kwa sasa Kiba anajipanga upya katika masuala hayo ya kupata mtoto na mrembo huyo.

Chanzo: Global Publishers
Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mmmh hakuna cha mimba wala mimbu
    kick kick tuu izo mjini apa
    tushawazoea

    ReplyDelete
  2. sijui ila kwa mtazamo wangu naona jokate angependeza kuwa mwanasiasa au mwanaharakati flani iv katika jami mziki naona kama hauwezi iv anatumia nguvu nying pasipo faida yoyote anajaribu kuwa kama vanesa lkn hawezi
    mtazamo tuu lkn

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad