Baraka Da Prince Amruka Kimanga Nisha..Adai Hana Uhusiano Wowote wa Kimapenzi na Nisha

Hatimaye Baraka Da Prince ameweka wazi kuwa hakuna uhusiano wowote wa kimapenzi na Staa wa Bongo Movie Nisha ila mashabiki ndiyo wanakuza mambo.

Baraka amesikika kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Afrika Radio,  akisema yeye na Bi dada ni washikaji tu na wamekuwa wakionekana sehemu mbalimbali pamoja ndiyo maana watu wanasema ni wapenzi.

“Siko kwenye mahusiano offcorse na hata kama ningekuwa kwenye mahusiano sijawa  tayari kuzungumzia mahusiano yangu”

Alisema Baraka na kuongeza
“Nisha Mimi ni rafiki yangu bana,ni mtu ambaye nipo naye muda mwingi,hivyo sina mahusiano yoyote na Nisha”

Ameongeza pia kuwa Watu wamekuwa wakimpakazia mara kibao kuwa ana mahusiano na Watu wakati si Kweli, Baadhi ya wasichana baraka aliowahi kutajwa kuwa nao kwenye mahusiano ni Agness Masogange na Menina.

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Jitu lenyewe bayaaa kama zimwi...

    ReplyDelete
  2. W.wake sisi tunatabu hatuchagui awe Na nanii tuu ashindilie basi chaaaa hongera anaitwA m.ume

    ReplyDelete
  3. mbayaaaaaaaaaa kama Teeeeeeeeeeeeee!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad