Hivi Ndivyo Zitto Kabwe Alivyosimamisha Bunge Baada ya Kutoa Hoja ya Kupinga Kutokuonyesha Vipindi vya Bunge

Zitto Kabwe
ZITTO KABWE ALISIMAMISHA BUNGE.Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe amelisimamisha Bunge kuanzia Saa tano asubuhi mpaka saa kumi jioni.Baada ya kutoa Hoja ya kumpinga uamuzi wa serikali wa TBC 1 kutokuonyesha vipandi vya Bunge.Hoja ambayo ilitolewa na Waziri Nape Nnauye;ndipo Zitto Kabwe akasimama na kuitaka Serikali iondoe hoja Hiyo Kwani TBC 1 ni shirika la Umma ambalo linaendeshwa kwa kodi za Wananchi.Zitto Kabwe ameungwa mkono na 70% ya Wabunge wote.Hivyo Serikali inatakiwa ije majibu.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mheshimiwa rais wa awamu ya tano john pombe magufuli aliwahi kuwaambia mawaziri aliowateua wasifurahie sana kuteuliwa,vinginevyo wakifurahia basi pia wawe tayari kufurahia watakapofukuzwa kazi.nina imani hili litatimia hivi punde kwa waziri wa habari na michezo nape nauye.nauye anamharibia vibaya mheshimiwa magufuli.kwa mwelekeo huu wa udikteta,ubabe,matumizi mabaya ya madaraka nape ameshaonyesha wazi kuwa hafai,hafai.nape kalifungia gazeti la mawio 'maisha' yaani milele.hata madikteta wakubwa wa dunia hitler wa ujerumani na mussolini wa italy hawakuwahi kuthubutu kuwanyamazisha wanahabari hivyo,ni maajabu mapya ya ukatili tanzania.tena leo kama haitoshi anatoa amri redio na televisheni ya taifa TBC kuacha mara moja kurusha matangazo ya moja kwa moja toka bungeni.maana yake nini? ni wazi tuu waandishi wake wafanye shooting,wakae chini na wahariri wao wachambue,wa-reedit makali wayaondoe na yabaki yanayoishabikia serikali tuu,kisha wayatafutie muda muafaka kuyarusha. JAMANI WANANCHI WENZANGU MATANGAZO YA MOJA KWA MOJA BUNGENI YALIANZA KURUSHWA MWAKA 2005,MIAKA 12 ILIYOPITA!huu ni uzandiki uliopindukia.ni fedheha na aibu.serikali inayaogopa maoni ya wabunge au inaficha wananchi wasizione amri za spika ndugai na mwenyekti wa bunge chenge wanapoamuru polisi wenye silaha kuingia bungeni na kuwaweka wabunge wa upinzani chini ya ulinzi?tunayaona,tunashangaa,tunalaani mno.TUNALAANI KWA NGUVU ZETU ZOTE. , mwisho kwako mhe.magufuli,salaam.kwa heshima na uungwana mkubwa tunatoa ombi rasmmi kwako.TUNAOMBA MFUKUZE KAZI NAPE NNAUYE.

    ReplyDelete
  2. Bado yupo kwenye CCM ya Kimwete. Wana maslahi na ndio hawa watumbuliwe vikali. Ndio hawa wLiohujumu nchi. Walimchague atekeleze haya. Kuyalinda na kutetea maslahi ya vigogo vya CCM. Hawaondoki kwa hiari. Hawalipi jodi , ushuru kwa hiari. WLizoea kwenda nje, muwLeta wawekezaji muwapa nchi, muwZuia na kuwanyanyasa Watanzania, huku wKiwa na maslahi yao. Ona uda, una shirika la nyumba, maduka ya luxury. Wanaogopa watanulikana wanafunga na kudai wamefirisika.wanafungia uhuru wa waandishi, funga magazeto yanayowTum u, nyanyasa wapinzani. Hapa kikomo. Magufuli si Mimwete. Hana mjomba wala shemeji. Ni tum ua tu.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad