Kocha wa Manchestet United Afunguka Kwa Uchungu 'Sipo Tayari Kujiuzuli'

Meneja wa klabu ya Manchester Louis van Gaal amesema kwasasa hana mipango ya kujiuzulu kutoka katika wadhifa wake na kushutumu sana habari ambazo zimekuwa zikienea kwenye vyombo vya habari.

United hadi sasa wameshinda mechi tatu pekee kati ya mechi 13 walizocheza karibuni ligini na katika shindano la kombe.

Van Gaal na wachezaji wake walizomewa na mashabiki baada ya kufungwa 1-0 na Southampton Jumamosi katika mechi ya Ligi ya Premia jambo hilo lililofufua tena uvumi kuhusu hatima yake.

“Ni mara ya tatu kwangu kufutwa (kwenye vyombo vya habari) na bado niko hapa,” amesema Van Gaal. United wamo katika nafasi ya tano ligini, alama 10 nyuma ya viongozi Leicester City zikiwa zimesalia mechi 15.

Manchester United watakuwa ugenini dhidi ya Derby County katika raundi ya nne ya Kombe la FA Ijumaa.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad