Kupotea Kimuziki Kwa Saida Kalori Kulisababishwa na Mambo Haya-Mrisho Mpoto

Mrisho Mpoto amedai kuwa moja kati ya sababu zilizofanya kupotea kwenye muziki kwa msanii wa nyimbo za asili, Saida Kalori ni kukosa uongozi mzuri wa kusimamia kazi zake.

Akizungumza kupitia kipindi cha Sunrise cha Times FM Ijumaa hii, Mpoto alidai kuwa msanii huyo hakuwa na usimamizi mzuri japo alikuwa na uwezo mkubwa kwenye sanaa.

“Ilifika kipindi kila kitu akawa anafanya yeye mwenyewe, hakuwa na uongozi mzuri sana, lakini naamini akisimamiwa hata sasa atarudi vizuri tu” alisema Mjomba.

Katika ‘line’ nyingine, Mrisho amewataka Watanzania kuzikumbatia tamaduni zao na kuachana na umagharibi, kwani kufanya hivyo ni sawa na kupigwa ‘pingu’ za akili.

Wakati huo huo Mpoto ambaye ameachia wimbo mpya uitwao Sizonje hivi karibuni amewataka mashabiki wa muziki wake kumpigia kura kwenye tuzo za Kora.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad