Mapya Yaibuka Kujiuzulu Katibu Mkuu wa Yanga...Yadaiwa Ameshinikizwa na Yusuph Manji

Baada ya uvumi kuenea kwa zaidi ya siku mbili sasa juu ya hatma ya katibu mkuu wa klabu ya Dar Es Salaam Young Africans Dk Jonas Benedict Tiboroha kuwa kajiondoa klabuni hapo na taarifa kuripotiwa kuwa huo ulikuwa ni uvumi, Jumamosi ya January 23 katibu mkuu wa Yanga Dk Jonas Benedict Tiboroha anaripotiwa kutangaza kujiuzulu nafasi hiyo.

Tiboroha anaripotiwa kujiuzulu kwa shinikizo na wala sio uamuzi wake binafsi, hivyo mchana wa leo January 23, baadhi ya wanachama wa Yanga wamekusanyika klabuni hapo wakilalamika na kumtuhumu mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuph Manji kuwa amemshinikiza katibu ajiuzulu baada ya kupewa maneno na baadhi ya watu na kumshinikiza Tiboroha ajiuzulu
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad