Mbwana Samatta Aeleza ni Kwanini Ameamua Kuichagua Jezi Namba 77 Kwenye Timu yake Mpya

Mbwana Samatta Akionyesha Jezi yake Mpya
Baada ya mchezaji wa Timu ya taifa ya Tanzania ya mpira wa miguu “Taifa stars” na mchezaji wa kimataifa Mbwana Ally Samatta kusaini mkataba wa miaka minne na klabu yake mpya GENK FC ya nchini Ubelgiji wa kuichezea soka klabu hiyo, alitambulishwa kwa waana habari kama ishara ya utambulisho rasmi wa Samatta klabuni hapo.

Katika utambulisho huo Samatta alikabidhiwa Jezi nambari 77, wakati katika klabu yake ya zamani ya TP Mazembe jezi yake ilikuwa nambari 9 mgongoni, jambo ambalo Mbwana Samatta alilazimika kulitolea ufafanuzi baada ya kutafutwa kwa njia ya simu kwenye kipindi cha Sports Bar ya Clouds TV, ambapo mbwana samata alijibu kuwa yeye anapenda jezi 7 lakini kwakuwa jezi hizo katika klabu nyingi huwa zimesha chukuliwa aliamua kuomba jezi nambari 77 kwakuwa aliamini ni mara chache watu kuitumia.

Samatta aliongeza kuwa hata wakati alipokuwa akiichezea TP Mazembe alikuwa akiushawishi uongozi umpatie jezi nambari 7, alkini haikuwa raihisi kwa kuwa ilikuwa na mtu tayari, na hivyo katika klabu yake mpya ya GENK FC hakuona sababu ya kuomba tena jezi hiyo badala yake aliamua kuomba jezi nambari 77 kwakuwa bado ana mapenzi na namba 7.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad