Msimamizi Wa BomoaBomoa Dar Aanguka Ghafla Ofisini Kwake.... Madaktari Washindwa Kubaini Tatizo

Operesheni kubwa ya kubomoa nyumba zaidi ya 15,000 zilizojengwa katika maeneo yasiyostahili jijini Dar es Salaam, imekumbana na changamoto ya aina yake baada ya mmoja wa wasimamizi wa kazi hiyo kutoka Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (Nemc), Heche Suguti, kuanguka ghafla akiwa ofisini kwake na kuwahishwa hospitali akiwa hoi.

Chanzo  kutoka ndani ya Nemc kimesema kuwa Suguti ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Sheria katika baraza hilo, alianguka ofisini kwake majira ya saa 9:30 alasiri baada ya kurejea kutoka katika Mahakama Kuu kitengo cha ardhi kushughulikia kesi inayoikabili Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi dhidi ya wakazi 681 wa eneo la Mkwajuni, Kinondoni ambao wanapinga nyumba zao kubomolewa.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa baada ya Suguti kuanguka ghafla ofisini kwake eneo la Mikocheni, baadhi ya wafanyakazi wenzake (wa Nemc) walimsaidia haraka kwa kumbeba na kumpakiza kwenye gari na kumpeleka hospitali mbili tofauti ambako kote vipimo vya awali havikubaini tatizo.

Baadaye alipelekwa katika Hospitali ya Aga Khan ambako alilazwa kuanzia siku hiyo (Jumanne) na kutolewa leo asubuhi (jana) baada ya kupata nafuu… ila kwa kifupi ni kwamba afya yake imeyumba na hadi sasa madaktari bado wanachunguza kujua ni kitu gani hasa kinachomsumbua,” chanzo kiliiambia Nipashe jana.

Mkurugenzi wa Nemc, Bonaventure Baya, alikiri kuwa Suguti aliugua baada ya kuanguka ofisini Jumanne wiki hii na kulazwa katika Hospitali ya Aga Khan, lakini haoni kama ni sahihi kuzungumzia afya yake kwani hayo ni masuala binafsi.

 “Nadhani ni uchovu ndiyo uliokuwa unamsumbua… hata hivyo, hayo ni masuala binafsi.  "

Alipotafutwa kwa njia ya simu jana mchana, Suguti aliyekuwa akizungumza kwa taabu, alikiri kupatwa na tatizo asilolifahamu na kuanguka ofisini kabla ya kujikuta akiwa amelazwa katika wodi mojawapo ya Hospitali ya Aga Khan.

Kwakweli sielewi kilichotokea. Nilipoingia ofisini kwangu baada ya kutoka kwenye kesi ya nyumba za watu wa Kinondoni, ghafla nikahisi kizunguzungu, giza kutanda na mwishowe nikaanguka… sijui kilichotokea baada ya hapo ila fahamu ziliponirudia nikajikuta nikiwa hospitali,” alisema Suguti.

Alipotakiwa kueleza zaidi kuhusiana na tukio hilo, Suguti hakuwa tayari kwa maelezo kuwa bado hajisikii vizuri.

Kwa sasa naomba uniache tu, sijisikii kuzungumza zaidi,” alisema na kukata simu.

Zaidi ya nyumba 16,000 zimeshawekwa alama ya X katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambazo zinatakiwa kubomolewa kutokana na kujengwa maeneo hatarishi.

Post a Comment

5 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. ndumba hizo mwenzio Yusufu makamba alipinda mdomo!

    ReplyDelete
  2. Hizo ni stress za majukumu yanayomkabili hakuna kumpuzika kushinda juani/ofisini(kikazi)kukosa kulala masaa ambayo binadamu anatakiwa alale kila siku(kiafya) waswahili msilete mambo ya kuamini imani zenu potofu za giza

    ReplyDelete
  3. Na bado watakufa wengi
    Mnaoenea watu masikini
    Mungu wape laana Na vilema vya maisha wote wanabomoa nyumba za watu bila kuwapatia makazi mengine
    Imekuwa dhambi kuwa masikini

    ReplyDelete
  4. Haiwezi kuwa ndumba kwani watz ni waelewa sana kuwa kazi anayofanya sio ya kwake bali katumwa.

    ReplyDelete
  5. Inshalla mwenyezi mungu atawaalani kwa kuongea watu kubomolewa nyumba zao watakuja kwa laana

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad