Mwigulu Nchemba Atumbua Majipu Mengine Iringa......Awasimamisha Kazi Viongozi wa Vyama vya Msingi vya Tumbaku

Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Mifugo, Mwigulu Nchemba amewasimamisha kazi viongozi wa vyama vya msingi vya tumbaku mkoani Iringa wanaotuhumiwa kushiriki katika ufisadi wa mkopo wa matrekta tisa kupitia mgongo wa vyama vya msingi vya wakulima wa tumbaku na kujimilikisha wenyewe.

Nchemba alifikia hatua hiyo jana baada ya wakulima wa tumbaku kulalamikia viongozi wa vyama hivyo na kuwataka wakabidhi ofisi.

Awali, mwanachama wa Chama cha Msingi cha Mfyome, Francis Kilatu alisema Benki ya CRDB inawakata fedha zao huku wamiliki wa matrekta hayo wakiwa ni wengine hivyo alimuomba waziri kulishughulikia mara moja.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mssikini mweee huruma yajulikana sasa yaliyofanywa miaka ileee

    ReplyDelete
  2. Mapambano bado yanaendelea

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad