Ukishindwa Kumnyonyesha Mtoto Miezi Sita Bila Kumpa Kitu Chochote, Andaa Pesa ya Tuition

Jamani kumekuwa na tabia ya watu kuwa busy na kushindwa kuwanyonyesha watoto kwa miezi sita bila kuwapa kitu chochote, hili ni kosa na tatizo kubwa sana kwa jamii.

Utafiti unaonyesha watoto wanaonyonyeshwa miezi sita bila kula kitu chochote wanakuwa na kinga imara dhidi ya magonjwa na ubongo mkubwa ukilinganisha na wale wanaoanza kupewa chakula au maji kabla ya muda huo.

Andaa pesa ya tuition kama utashindwa kumnyonyesha mtoto miezi sita mfululizo bila kitu chochote hata kama umempeleka international schools.

Wanawake msiwe busy sana na kazi na kusahau wajiu wenu wa malezi. Lakini pia ni vyema wenza kujipanga vizuri kabla ya kuzaa mtoto ili akizaliwa apate malezi mazuri.

Ukitaka mtoto mmwenye afya imara na akili nyingi anza kwa kumuandaa mke wako kabla ya kumpa mimba na pia lea mimba kwa upendo na uaminifu mkubwa. mkinge mkeo na magonjwa yanayozuilika akiwa mjamzito. Baada ya mimba mpe malezi mazuri akizaa mpaka miaka miwili kwa maana ya chakul.

Nawaasa watu kuuiga pia utamaduni wa wachaga katika kulea mke akizaa na utamaduni wa wairaq katika kulea mimba..
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad