Mwalimu Mkuu Ashushwa Cheo na Kukamatwa na Takukuru Kwa Rushwa ya KUKU

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Amani Mwenegoha amemvua wadhifa wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Sinamila, Mashaka Lusotola na kumrudisha kuwa mwalimu wa kawaida.

Hatua hiyo ilikuja baada Mwenegoha kubaini kuwa walimu wa shule hiyo wamekuwa na tabia ya kuwaagiza kuku, wazazi wanaowaandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza.

Mwenegoha alichukua maamuzi hayo, baada ya kuthibitisha kuwa mwalimu huyo mkuu, ameshindwa kudhiti tabia hiyo ya walimu walio chini yake.

Akizungumzia kusimamishwa kwake, Mwalimu Lusotola alisema amefurahi na kufananisha adhabu hiyo na kumpiga teke chura.

Tayari mwalimu huyo amekamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupamaba na Rushwa (Takukuru), leo anatarajia kwenda kuandikisha maelezo, huku akisisitiza kuwa hajaomba kitu chochote kwa wazazi.
Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ni aibu sana kwakweli. Sasa admn naomba unipe maelekezo jinsi ya kusajiri blog kwenye vidokezo.com app.kama ulivyofanya wewe

    ReplyDelete
  2. Magufuli kazi unayo kuku kuku kuku wengine wanatoka jela kwa kuiba mabilion eti kwenda kufagia hospitali
    Fyuu Magufuli Na CCM yako
    Tutaiba sana kwani tunajua mwishoni tutafagia mahospitali

    ReplyDelete
    Replies
    1. WW jidanganye Tu, utaacha familia yko ikiteseka na kukulilia hizi zama nyingine kama unajijua Ni jipu jiandae soon utakutoka usaha

      Delete

Top Post Ad

Below Post Ad