Nay Wa Mitego anusurika kutekwa,Je kisa ni wimbo wa Shika adabu yako?

Msanii wa Nay wa Mitego ambaye kwa sasa yupo kwenye seke seke baada ya kuachia wimbo wake wa shika adabu yako ambao amewa diss watu wengi maarufu, siku kadhaa zilizopita alinusurika kutekwa na watu wasiojulikana.

Nay amekiambia kituo kimoja cha redio kuwa kuna siku alikuwa anatoka studio akaona gari limekuja kupaki nyuma ya gari lake,alipoanza kutoka gari hilo likaanza kumfuatilia kwa nyuma kila ndipo hapo alipoanza kutia mashaka.

Nay amesema kuwa alipata mashaka zaidi baada ya kuona kuwa gari hilo linazidi kumfuata hata baada ya kujaribu kubadilisha uelekeo aliokua kuwa akienda ndipo alipoamua kuwapigia marafiki zake ili waje kumsaidia.

Nay anasema baada ya kuzunguka sana ili kuwakwepa watu hao mwishowe alifanikiwa kufika manzese usiku sana kwa masela wake na kukuta amepishana nao kwa vile walikwenda kumfuata,akibidi awapige warudi haraka na ndipo hapo ilikuwa ponea yake.

Nay amesema anahisi vugu vugu la wimbo wake wa shika adabu yako linaweza likwa ndio chanzo na pia amesema anafanya mipango ya kujilinda zaidi.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. unajidai mjanja kumbe unaogopa mpaka kivuli chako,,..acha uoga we si unajidai kidume ungesimamisha gari upigane. unataka kujamba wakati unaharisha utajiharishia tu.

    ReplyDelete
  2. Na bado, mpaka uombe poooooo.... UTRAJUTRAA KUSHUKA DALADALA KWA MGUU WA KULIA.........!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad