Shilole Amkana Nedy Music, Asema Sio Mpenzi wake...Agoma Kumzungumzia Demu Mpya wa Nuh

Mwanadada anayetamba kwenye muziki wa bongo fleva na bongo muvi,Shilole amekana kutoka kimapenzi na msanii anayechipukia kwenye bongo fleva,Nedy Music.

Akihojiwa na redio moja Shilole amesema kuwa msanii huyo ni mshikaji wake tu hakuna kinachoendelea baina yao na kukanusha kuwa msanii huyo anaishi nyumbani kwake.

“Nedy music ni mshikaji wangu..anakaa kwake mimi nakaa kwangu.Mimi ni mwanamke mtafutaji kwa hiyo mambo ya mapenzi siyaweki saana,nafocus kwenye kazi” alifunguka Shilole.

Alipoulizwa kuwa inasemekana mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda ameopoa demu mkali kuliko yeye,Shilole alikataa kata kata kuzungumzia hilo na kusema hana muda wa kumwongelea mtu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad