Tetesi za Kutimuliwa kwa Van Gaal zashika Kasi...

Kocha mkuu wa klabu ya Manchester United Louis Van Gaal huenda akatupiwa virago na nafasi yake kuchukuliwa na Jose Mourinho kabla ya mwisho wa mwezi Februari kwa mujibu wa gazeti la The Sun.

Kipigo cha 2-1 kutoka wa Sunderland Jumamosi kumewaacha mashetani wekundu na nafasi ndogo sana kumaliza nafasi ya nne msimu huu huku Ligi ya Uropa ndiyo michuano pekee wanayoweza kufuzu kwa ajili ya msimu ujao kucheza klabu bingwa barani Ulaya.

Mourinho amekuwa akitajwa sana kwenye tetesi za kibarua cha Man United licha ya nadharia zilizozuka kuwa huenda asiendane na tamaduni za klabu hiyo.

Inaaminika kuwa kwa hali hii hawawezi kutinga nne bora kabisa huku habari zinadai kuwa uongozi wa mashetani hao wekundu unaweza kusitisha mkataba wa Van Gaal na kumleta Mourinho sasa wakati wakilenga mechi dhidi ya Arsenal Februari 28

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad