A.Y Afunguka Sababu ya Kumfanya Meneja wa Diamond Awe Meneja Wake Pia....Sababu Ipi Hiyo?

Mkongwe AY amefunguka sababu kubwa ya yeye kumfanya Salaam,meneja wa diamond kuwa meneja wake pia ni kutokana na kuzidiwa na majukumu.

A.Y amefunguka kuwa hajawai kuwa na meneja kwenye maisha yake ya muziki lakini amemchagua Salaam kwa kuwa anaujua utendaji wake kwani wamekuwa toka wadogo na anahisi anaweza kuvaa viatu hivyo.

“mpaka mimi nimefika hapa leo sikuwahi kuwa na meneja kwa hiyo naona kama kazi zinakuwa nyingi lazima nipate msaidizi mwingine,nikaona Salaam ndiye mtu anayeweza ku fit kwenye hivyo viatu” alifunguka A.Y na kubainisha kuwa amewahi kufanya kazi na meneja huyo lakini haikuwa rasmi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad