Harmonize Afunguka Kwanini Hajawai Kufanya Show Dar..Adai Menejimenti yake ilimkataza

Msanii wa bongo fleva Harmonize ambaye yuko chini ya lebel ya Wasafi inayomilikiwa na Diamond amefunguka kuhusiana na yeye kutowahi kufanya show jijini Dar es salaam na kusema ni mikakati ya menejiment yake kum brand.

Msanii huyo ambaye ameachia wimbo mpya wa Bado amesema aliahidiwa kuanza show baada ya wimbo wa pili na pia kuna uwezekano wa kuachia album.

“Msanii lazima uji brand,muziki ni biashara na kila biashara ina misimamo na mikakati yake,ukiweka mikakati mibovu huwezi kuingiza faida.Halafu pia menejimenti yangu ilinambia the way tunaku brand hatutaki ufanye show Dar es salaam kwanza mpaka ukitoa wimbo wa pili ndio utakuwa una uwezo wa ku perfom Dar es salaam na popote duniani” alifunguka Harmonize.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad