Harmonize Asema Haya Kuhusiana Beef ya Diamond na Ali Kiba....Amesemaje?

Msanii wa bongo fleva,Harmonize ambaye yuko chini ya lebel ya wasafi inayomilikiwa na Diamond amefunguka na kusema yeye hajui kama kuna ugomvi wowote kati ya bosi wake na Ali Kiba kwani hajawai kusikia akimzungumzia vibaya msanii huyo.

Harmonize pia ameenda mbali na kusema kuwa yuko tayari kufanya kazi na Ali Kiba kama itatokea kwani ni moja kati ya msanii mkali.

“Mimi sijui kama kuna beef,sijawahi kumsikia Diamond akimwongelea msanii yeyote tofauti..Diamond ni kati ya watu wanao support muziki wa Tanzania,ukiona kolabo nyingi za wasanii wa Tanzania na nje Diamond ana Mchango wake” na kuendele kusema kuwa yuko tayari kufanya kazi na Kiba “Ali Kiba ni msanii mzuri,kwa hiyo kolabo ikiwa na tija nitafanya naye“.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad