JOYCE KIRIA Amchimba Mkwara Mume Wake...Atishia Kumpiga Chini Asipofanya Haya

Mtangazaji wa Kipindi cha ‘Wanawake Live’ kinachorushwa kupitia Televisheni ya East Africa, Joyce Kiria amefunguka kuwa hata kama mumewe wa ndoa hatakuwa mchapakazi atampiga chini na kuendelea na maisha mengine.

Akizungumza na mwandishi wa habari, Joyce, ambaye leo anazindua rasmi kampeni yake ya ‘Mwanamke Piga Kazi’ inayofanyika katika Viwanja vya Leaders jijini Dar, alisema kuwa kwa kipindi ambacho tupo nacho sasa hivi lazima kupiga kazi.

“Kwangu, hata kama mume naye atakuwa mzembe wa kupiga kazi nampiga chini kabisa maana sasa hivi tunakimbizana na kazi ya kupiga kazi kwa nguvu ili tuwezeshe kusonga mbele zaidi,”  alisema Joyce.

Pia mtangazaji huyo aliongeza kuwa anawaomba wanawake wengi wajitokeze kwani hakutakuwa na kiingilio chochote, lengo ni kuja kujifunza mbinu za kujikomboa kama wanawake na kujiamini katika kufanya kazi.

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kila la kheri dada Kiria.

    ReplyDelete
  2. Huyu dada naye ana kiherehere huyuuuuu, kazi zenyewe ziko wapiii????? Hawa ndio aina ya wale wanawake wanaowawekea pressure za maisha majamaa zao mpaka mwisho wa siku wanaanza kuiba na kufanya ufisadi halafu wakitumbuliwa wao ndio haooooo wanaruka kimanga.......hovyoooooooooooooo mxieeeeeeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  3. Hetariiiiii napita tu naelekea kirua vunjooo

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad