Lulu Michael Afunguka...Mastaa Wengi Bongo Mtaishia Kuchambana Instagram

ZA uso laivu! Staa mwenye mvuto Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa mastaa wengi Bongo wataishia kuchambana kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram badala ya kutafuta elimu ili siku moja wapate nyadhifa serikalini.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita, Lulu alisema kwamba, amegundua kuwa elimu ndiyo kila kitu hivyo amewasihi mastaa wenzake waache kuchambana na kutuma picha kwenye mitandao ya kijamii badala yake watafute njia ya kujikwamua kielimu.

“Jamani mmemuona mwanamama mwenzetu Dk. Tulia alivyojinyakulia unaibu spika? Hiyo ndiyo raha ya elimu. Mastaa kazi kutukanana kwenye mitandao ya kijamii na kuweka picha, mwisho wenu utakuwa hivyohivyo,” alisema Lulu.

Chanzo: GPL

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. pia mtaishia kuacha wazi maungo yenu na kuyaanika nje iliwateja wajionee kama hicho kifua na makwapa vyote ni dhahiri njenje. biashara matangazo

    ReplyDelete
  2. Bora wanaolongana mitandaoni kuliko wewe mchawi

    ReplyDelete
  3. Bora Mchawi kuliko Muongo

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad