Mbowe Kuzungumza na Taifa Kupitia Waandishi wa Habari Makao Makuu CHADEMA Leo

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe leo atazungumza na Taifa kupitia mkutano wa waandishi wa Habari.

Mkutano huo wa waandishi utafanyika saa 6 mchana makao makuu Kinondoni Ufipa.

Kiongozi huyo mkuu wa upinzani nchini anatarajiwa kutoa tamko rasmi la maazimio ya Kamati kuu ya chama iliyokutana Machi 1

Tayari vyombo vya ndani na nje ya nchi vimealikwa kwenye mkutano huo na imetakiwa ifikapo saa 5 asubuhi waandishi wote wawe wamekaa kwenye nafasi zao.

Mwenyekiti huyo anabashiriwa mbali na mambo kadhaa lakini atatoa msimamo rasmi wa chama kuhusiana na hujuma ya watawala dhidi ya uchaguzi wa meya wa DSM

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Umeya sio kitu cha msingi tupe dira ya chama kuelekea 2020 na nani mrithi wa Slaa

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad