Nyumba ya Mzee Katwila Yamuua Bibi Yake Mwanamuziki Q Chief

Mwanamuziki wa Bongo fleva, Q Chief, yupo kwenye majonzi baada ya kumpoteza Bibi yake aliye fariki kwa mstuko wa moyo baada ya misuko suko ya madeni na kutolewa kwenye nyumba baba mzazi wa msanii huyo Mzee Shaaban Katwila.

E-newz imekutana na mmiliki wa Q S Entertainment inayomsimamia Q chief ijumaa iliyopita katika onesho la band ya QS Band pale Escape One. QS J. Mhonda na kutufahamisha makubwa yaliyomkuta Bibi yake Q chief upande wa mama aliposikia taarifa ya nyumba kuchukuliwa na mtu anayedai pesa alizomkopesha mzee Shaaban Katwila. Taarifa iliyopelekea bibi kupata presha na kuiaga dunia na mpaka kufikia siku ya Ijumaa Bibi yake na Q Chief akapumzishwa katika nyumba yake ya milele.

Mbali na yote hayo kutokea Q Chief alionesha ukakamavu na kupanda kwenye stage na kuendelea kutumbuiza siku ya ijumaa pale ESCAPE ONE.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad