Salim Jecha Aendesha Uchaguzi Kutoka Mafichoni Zanzibar.....

Hatimaye  uchaguzi mkuu wa marudio Zanzibar Umefanyika Jana huku Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (ZEC), Jecha Salim Jecha akishindwa kuonekana hadharani kuzungumzia uchaguzi huo.

Kwa kawaida, kama ilivyokuwa katika uchaguzi wa awali uliofanyika Oktoba 25 kabla ya kufutwa siku tatu baadaye, Jecha alitarajiwa kuwa mstari wa mbele na kuzungumza na waandishi wa habari kwa nia ya kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusiana na uchaguzi huo.

Hata hivyo, katika tukio nadra kuwahi kutokea hapo kabla, Jecha aliendelea kuadimika na hadi kufikia jana jioni, taarifa zake kwa umma zilitolewa kupitia taarifa iliyosambazwa kwa vyombo vya habari na wasaidizi wake tu huku yeye mwenyewe akiendelea kutoonekana hadharani.


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad