Zitto Kabwe Afunguka Tena Kuhusu Sakata la Rushwa Kamati za Bunge..Awataja Takururu...

Zitto juzi alitangaza kujiuzulu katika Kamati Bunge Huduma za Jamii aliyokuwa akihudumu kwa madai ya baadhi ya wajumbe kupokea rushwa.

Kupitia ukurasa wa mtandao wa kijamii wa 'Facebook' Mbunge Zitto amesema kwamba hatua inayochukuliwa na TAKUKURU ni hatua nzuri itakayopelekea ukweli kujulikana na watakaokutwa na makosa kuchukuliwa hatua stahiki.

''Uchunguzi wa vyombo vya dola ni moja ya njia muafaka ya kuhakikisha kila lisemwalo linakuwa na ukweli na pale ambapo suala limezushwa tu itajulikana na wazushaji hatimaye wataacha''-Amesema Zitto.

Aidha ikumbukwe kuwa baada ya tuhuma za rushwa katika kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii Mbunge Zitto Kabwe alimwandikia Spika wa Bunge Job Ndugai barua ya kujiuzulu akifuatiwa na Mbunge wa Nzega Mjini Hussen Bashe (CCM) ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo na ukweli uweze kufahamika.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad