Mr Blue Aibuka na Kumtuhumu Mh Sugu Kumuibia Wimbo wa Freedom..Ushahidi Kamili Huu Hapa

Msanii wa Bongefleva ambaye jina lake lilianza kushine kwenye game ya muziki wa Bongofleva toka akiwa na umri mdogo Mr. Blue, amerudi kwenye headlines baada ya kupost kupitia account yake ya instagram na kuelezea hisia zake kuhusu wimbo mpya alioutoa Mr. II Sugu kuwa ni wimbo ambao alimshirikisha na anashangaa kuona mambo yapo tofauti.

Katika post ya instagram Mr. Blue aliandika

“Ndugu zangu nipeni ushauri kwa hili niliona nikae kimya ila limeniuma sana kwa kweli ..!! SUGU namuheshimu km kaka yangu kimuziki na kiumri pia ..sasa kuna nyimbo nilimshirikisha inaitwa “Freedom” tulifanya pale kwa makochali na hiyo ndo picha ya ushahidi na nyimbo ipo youtube kwa wasioisikia..sasa kinachonishangaza leo kuona ameitoa verse yangu na kuweka verse zake mbili na kaishoot mpaka video na nyimbo imekuwa yake tena bila kunitaarifu mimi mwenyewe au ridhaa yoyote kutoka kwangu je hii ni haki kweli??? Maana mtu ukiongea unaonekana unatafuta kiki au sijui nn…mi imeniuma kwa kweli jamani je mnanishauri nini ndugu zangu….????”

Hii ndio video mpya Mr. II aliyoitoa leo April 25 2016 ‘Freedom’ na chini yake nimekuwekea wimbo wa Mr Blue Feat. Sugu
Wimbo wa mr Blue
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad