Msafara wa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo Wapotea Dodoma

Msafara wa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo leo asubuhi ulipotea njia kutokana na watumishi wa Manispaa ya Dodoma kutojua eneo ambalo waziri huyo alikuwa analitembelea.

Waziri Jafo alikuwa amepanga kufanya ziara kwenye Shule ya Msingi ya Nzuguni B kwa lengo la kuangalia mapungufu, hasa tatizo la uhaba wa madawati, lakini hakufika kama alivyotarajia kutokana na watumishi hao kutojua eneo ambalo shule hiyo iko.

Shule hiyo haijawahi kutembelewa na ofisa elimu tangu mwaka 2007 licha ya kuwa kilomita 6 kutoka katikati ya mji.

Naibu Waziri alikasirishwa na kitendo hicho akawataka watumishi wa idara ya Elimu wajipime kama wanastahili kuendelea kufanya kazi.

“Mstahiki Meya, mimi niliona wazi kuwa watumishi wako wananipoteza," alisema Waziri Jafo.

"Nimechukia sana na hawa watu. Tatizo lao ni kwamba hawajawahi kuja katika shule hii tangu mwaka 2007, lakini wamekaa ofisini tu. Ikiwezekana waondolewe na kupelekwa vijijini,” alisema Jafo.
Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hamna haja yakupelekwa vijiji hao futa kazi kwani kasi ya magufuli hawaiwezi

    ReplyDelete
  2. Majipu yatawaponza

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad