Mwanasiasa wa Upinzani Auawa Nairobi Kenya..

Mwanasiasa wa upinzani ameuawa kwa kupigwa risasi nje ya nyumba yake katika mji mkuu wa Kenya Nairobi.

Stephene Mukabana ambaye ni kiongozi wa vijana wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM), aliuawa usiku wa jana wakati alienda kumsaidia mtu mmoja aliyekuwa akiporwa na kundi la watu sita kwa mujibu wa gazeti la Standard nchini humo.

Pia gazeti la Standard lilimnukuu gavana wa Nairobi Evans Kidero akisema kuwa kundi la wauaji limfuata na kumuua mwanasiasa huyo wa umri wa miaka 42.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad