Rais Magufuli Atoa Somo Kwa Waandishi wa Habari..Awaomba Waitangaze Tanzania..Majirani Waache Kutangaza Maliasili za Tanzania Kuwa ni zao

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo juzi wakati wa uzinduzi wa Daraja la kisasa la Kigamboni ambalo litakua mfano Afrika mashariki, huku akiwaomba Kuandika kwa kuitangaza nchi Kwanza

Dkt. Magufuli amesema kuwa kama waandishi wasipoitangaza Tanzania hakuna mwingine wa kuweza kufanya hivyo na ndio maana hata nchi jirani wanadiriki kunadi maliasili za Tanzania kuwa zinapatikana nchini kwao.

Aidha rais Magufuli amewaomba wahariri wa habari kuweka kurasa za mbele habari za maendeleo pia sio kila baya ndio ziwe katika ukurasa wa mbele bila kujali mazuri yaliyofanyika kwa wakati huo.

“Kwa ndugu zangu waandishi ninawaomba muitangaze Tanzania, muitangaze Tanzania mmuipende Tanzania, tusiwe wepesi wa kuandika mabaya tu ya Tanzania kila baya lipo kwenye front page zuri hakuna”Rais Magufuli alisema

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. MAJIRANI WATATUKOMA MWAKA HUU, WATATANGAZA BAHARI YA HINDI KUWA YAKO....hahahahahahaha

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad