Rooney Ndiye Mwanamichezo Tajiri Kwa Uingereza, Wengine ni ..

Gazeti La Sunday Times limemtangaza Wayne Rooney kama mwana michezo tajiri nchini Uingereza.

Rooney ambaye ni mchezaji wa timu ya Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza, ndiye mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa kwenye ligi ya uingereza akipokea paundi 300,000 kwa wiki.

Rooney ameingia kwenye list hiyo baada ya kuwa na utajiri wa paundi milioni 82 na kuwazidi wanamichezo wengine wan chi hiyo Andy Murry mwenye utajiri wa paundi milioni 58 na Rory McIlroy mwenye utajiri wa paundi milioni 56.

Rooney amefanikiwa kuongeza paundi million kumi kwa mwaka huu kwenye utajiri wake kutokana na kuwa balozi wa Nike na Samsung.

Hii ni list ya top ten ya wanamichezo matajiri wa Uingereza:

1.Wayne Rooney Football, Manchester United £82m

2 .Andy Murray Tennis £58m

3.Rory McIlroy Golf £56m

4.Gareth Bale Football, Real Madrid £34m

5.Sergio Aguero Football, Manchester City £33m

6.David Silva Football, Manchester City £31m

7.Cesc Fabregas Football, Chelsea £29m

7.Radamel Falcao Football, Chelsea £29m

9.Samir Nasri Football, Manchester City £22m

10.Eden Hazard Football, Chelsea £18m

11.Amir Khan Boxing £18m
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad