TANZIA: Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Christina Lissu Afariki Dunia Jijini Dar

Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum toka Singida, Christina Mughwai Lissu(CHADEMA) amefariki dunia kwa ugonjwa wa kansa.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa cancer tangu mwaka jana.

Tundu Lissu Ameandika Hivi:



Waheshimiwa nawasalimu kutoka Kibondo.

Nina habari zisizokuwa njema. Dada yangu na aliyekuwa Mbunge wetu wa Viti Maalu m Mh. Christina Lissu Mughwai amefariki dunia muda mfupi uliopita katika hospitali ya Aga Khan Dar.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa cancer tangu mwaka jana.

Kwa sasa niko nje ya Dar na ndio kwanza taarifa hizi zimenifikia, sina taarifa zaidi juu ya mipango ya mazishi, etc. Tutawataarifu baada ya familia kuwa tumeshauriana.

Tundu Lissu.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad