TETESI:Anne Kilango Kupangiwa Kazi Nzuri zaidi ya Ukuu wa Mkoa Aliyofukuzwa

Mh Anne Kilango Maleccela anasubiri kupangiwa kazi nyingine na Rais Dr Magufuli na huenda akapangiwa kazi nzuri zaidi ya kazi yake ya awali ya Ukuu wa Mkoa.

Kuna baadhi ya taarifa zinasema kwamba huenda akateuliwa kuwa balozi katika mojawapo ya nchi za ng’ambo.

Ofisa mmoja wa Ikulu ambaye hakupenda kutajwa jina lake alinukuliwa akisema kuwa “Rais Magufuli anajiandaa kumpangia Kilango kazi nyingine na kuna uwezekano mkubwa akateuliwa kuwa balozi katika nchi za Ulaya, Marekani au Asia”, alisema.

CHANZO: Gazeti la ZANZIBAR YETU


MAONI YANGU

Rais Maguguli anajua sana kucheza na akili za watanzania. Staili yake ya utumbuaji majipu imenjengea umaarufu kwa wananchi kiasi kwamba kila jambo analofanya, liwe zuri au baya, wananchi hushabikia tu kama jongoo pasipo kuelewa mantiki na manufaa yake kwa umma wa watanzania.

Wakati watanzania wanamshabikia Magufuli kwa kutumbua JIPU kumbe ndio kwanza anafikiria kulipangia JIPU kazi nzuri na ya heshima zaidi ya Ukuu wa Mkoa. Nchi hii haiishi vituko.

Jamii Forums

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. NAOMBA SANA KWA MUNGU WANGU,HUYU MAMA NI JEMBE,MKUU AANGALIE NA UZITO WA KOSA LA KILANGO.NA IWE HIVYO KWA JINA LA YESU.

    ReplyDelete
  2. Ombeni sefue nae aliambiwa hivyo hivyo asubiri apangiwe kazi,nae huyo mama atasubiri sana.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad