Waziri Nape aufuta mchakato wa Vazi la Taifa. Ashauri kila kabila litumie vazi lake

Mhe. Nape Nnauye ametoa tamko la kuufuta mchakato wa kutafuta vazi la Taifa na kuagiza kila kabila litumie vazi lake.

Uamuzi huu alioutoa akiwa ziarani Singida, anasema umetokana na ugumu wa kupata vazi hilo, kukosa mifano ya nchi iliyofanikiwa kupata vazi kupitia mchakato kama wetu na zaidi ni enforcement ya uvaaji.

Akachekesha kwa kuhoji, "Kama uvaaji wake utakuwa ni kwa amri kama magwanda ha jeshi au ni hiari?"

Hivyo, kwa kauli yake huo mchakato umefikia ukomo wake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad