WAZO HURU:Kuikumbatia UCHINA ni Janga la Taifa Tutakuja Juta Siku Moja

Fikiria wachina waliofika kuuza mahindi ya kuchoma ndani ya jiji hata kufikia kuuza mafenesi pale mjini Muheza ,wachilia mbali kuingia katika biashara za vipusa ,but they dont care about us ,hilo mlijue.

Wachina wauza karanga na kwa jinsi tunavyowaonyesha paja ndivyo watakavyotaka tunyanyue nguo kamili ,kwa maana hiyo WaTanzania mjue biashara zenu zote watazikamata wao na hatutoweza kushindana kibei ,watauza bei poa kiasi ya wewe kula hasara na kuamua kumwaga manyanga ,leo hii wanajaliza biashara zao feki na huwapa wamachinga kuuza,hapa wanapima upepo tu ,muda si mrefu watauza wenyewe na hao wamachinga watabakia kufuta mavumbi bidhaa kwenye maduka ya wachina.

China ni Taifa lenye watu wengi na kwao hawana la kufanya siasa wanazotumia ni kuwasambaza wengine katika nchi za nje na huwapa kila msaada na kuwalinda kimaslahi ,tunapoanza kuitegemea China kimisaada basi mjue watatoa misaada kila rangi na kutudumaza akili kiasi ya kutufikisha kwenye point ambayo tutakuwa hatuwezi hata kuchamba bila ya kupata msaada wa kichina kwa msemo mwengine itakuwa tumeshanasa na tunakokotwa kama mbuzi anaegoma kuvutwa kamba.

Serikali inaona imepata kuwa ina/itapokea misaada kutoka china kumbe bila ya kuona mbali itakuwa imepatikana.

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. China wana matatizo lakini hawajasababisha matatizo na majanga makubwa yanayoendelea kuitafuna dunia kama vile, Mamilioni ya maisha ya watu yanayoendelea kupotea na kupoteza makazi yao kila siku kwa kisingizio cha demokrasia . Iraq,Afghanistan,Libya,Syria,
    Egypt na sehemu nyengine za dunia. Sasa hapo katika mifano hai michache mwenye akili timamu ataelewa na kutofautisha nani mtu wa majanga zaidi kati ya China na hao wengine wanaojifanya wazee wa demokrasia duniani.

    ReplyDelete
  2. China wamesawazisha Majangili, mafisadi, Tanzania, Malaysia, Indonesia, Zimbabwe, Afrika Kusini na sasa wanavutana na Philippines na Japani. Wanaokufa kwa kansa, magonjwa, n.k. ni wengi kuliko wa vita.

    ReplyDelete
  3. wachina kweli wameitawala Tanzania, kwani hawawezi kuuza mahindi inchini kwao? mimi naishi Ulaya siku moja nilikuja na simu origino za Nokia kuja kuuza bongo sikupata mnunuaji sababu wabongo wananunua simu za bei nafuu na feki za kichina

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad