John Terry Aongezewa Mkataba wa Mpya Chelsea

Klabu ya Chelsea imethibitisha kumuongezea nahodha wao John Terry mkataba mpya wa mwaka mmoja sasa ni juu yake kubaki au kuondoka Stamford Bridge msimu ujao.

Msemaji wa klabu amesema; “Marina Granovskaia na Bruce Buck wamekutana na John na wakala wake na kumpa ya Mkataba wa mwaka mmoja abaki,”.
“Na wakati msimu unaelekea ukingoni, haya ni maamuzi mazito kwa John na familia yake na kitu ambacho wanakifikiria kwa sasa,”.

Mashabiki wa Chelsea walikuwa wakimpigia debe Nahodha huyo usiku wa Jumatano Uwanja wa Anfield wakitaka Terry aongezewe Mkataba mpya huku wakiwa wamebeba mabango yanayoonyesha mataji mengi ambayo klabu ilishinda chini ya uongozi wake.

Pamoja na kwamba umri umeenda na kiwango kimeshuka, lakini Terry bado ni kipenzi cha mashabiki wa Stamford Bridge haswa wanapokumbuka mchango wake enzi zake.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad