Millen Magese Afunguka 'Watanzania Tupende vya Kwetu'

Mwanamitindo wa Kimataifa kutoka Tanzania anayefanyia shughuli zake nchini Afrika Kusini na Amerika, ametoa witoa kwa watanzania, akiwataka kuwa wazalendo.

Kwenye ukurasa wake wa Instagram Millen Magese ambaye kwa sasa yupo mapumzikoni Jijini Dar es Salaam, amendika ujumbe kwa watanzania akiwaambia kuwa na upendo na kuthamini vya kwao, pamoja na kuvitangaza, huku akielezea matamanio yake ya kwenda mbuga ya wanyama ya Serengeti na Saadani.

“Tuwe na utamaduni wa kupenda vya kwetu na kusifia vya kwetu, na kutangaza vya kwetu......Tanzania is beautiful ..... Tutembelee vya kwetu .#SmallVacayInTanzania, next....wish to go to Serengeti and Saadani, #TakingTimeOff”, aliandika Millen Magese.

Kwa sasa mwanamitindo huyo yupo kwenye kampeni kubwa ya kutafuta tiba ya ugonjwa wa endometriosis, ambao umemsumbua kwa miaka 13 mpaka sasa, uliopelekea kufanyiwa upasuaji mara 13 kupata matibabu yake.

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. na wewe Millen Magesse na wewe upende vya kwetu, sasa kwa nini unaenda kufanya kazi nchi nyingine wakati kazi ya uanamitindo bongo zipo kibao, unawasema wenzio tu lakini wewe mwenyewe upendi vya nchi yako du, watanzania bana huwa hawaeleweki, mpaka hata jina la kibongo la Happiness ukabadilisha ukataka kuitwa jina la kigeni, halafu unasema watanzania tupende vya kwetu wakati wewe mwenyewe hata jina la kwetu la Happiness hulitaki nani atakusikiliza, Millen, kiss my ass!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Umeuno eeh!Hata ngozi yake ya asili haitaki,full MKOROGO!

      Delete
  2. kama Lulu akisema tupende vyetu naweza kumuelewa kwani Lulu kazi zake anafanya bongo sio nchi ya nje kama Happiness au Millen Magese

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad