Penzi la Diamond, Kiba Lamtesa Jokate

Siri imevuja kuwa penzi la vinara wawili wa Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond PlanumZ’ na Ali Saleh Kiba ‘King’ linadaiwa kumtesa mlimbwende Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ ambaye amekuwa akijutia kujiingiza kwenye uhusiano na wasanii hao.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa Jokate, hivi karibuni alitupia mashairi ya Wimbo wa Ndi Ndi Ndi wa Mwanamuziki Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ kwenye ukurasa wake wa Instagram ambapo baadhi ya mashabiki wake walimtaka kuwaahidi kuwa hatarudia kujiingiza kwenye penzi la mastaa hao (yaani Diamond na Kiba) kwani ishu hiyo ilimfanya atafsiriwe vinginevyo tofauti na ilivyokuwa awali.
kiba jokate

Ilisemekana kuwa kauli hizo za mashabiki hao zilikuwa kama kugongelea msumari wa moto kwenye kidonda kwani ishu hiyo imekuwa ikimsumbua na kumsababishia maumivu yanatokana na kujutia uamuzi wake huo kwa kuwa hakudumu nao.
“Unajua Jokate alijijengea na ana heshima sana kwenye jamii yetu kwa uwezo na upeo wake (IQ) na hata kujitambua, sasa anapokuwa na uhusiano na msanii kisha baada ya muda mfupi akaachana naye kama ilivyokuwa kwa Diamond na sasa Kiba, inaweza kumshusha hadhi, na hiyo ndiyo inamfanya Jokate ajute kujiingiza kwenye mapenzi na mastaa hao,” kilifunguka chanzo hicho.


ALIPASWA KUWA BUNGENI?
Hata hivyo, baadhi ya watu wake wa karibu walikwenda mbele zaidi na kusema kwa muonekano wake alipaswa kuwa mjengoni (bungeni) akitema madini, kwani hawana hofu na elimu yake ila tatizo ni hilo tu la ‘kurukaruka’ na wasanii.
 “Kiukweli Jojo (Jokate) anastahili kuwa bungeni akitafuta njia mbadala ya kutatua matatizo ya wananchi wake wa jimbo lake f’lani hivi.
“Au kama anataka kuendelea na mapenzi kwa kuwa ameachana na Kiba basi atafute mtu wake na kutulia naye kwani kuna baadhi ya warembo wenye majina wana watu wao na wametulia wanafanya mambo ya kujenga taifa,” alisema mmoja wa watu hao.

HUYU HAPA JOKATE
Baada ya kunyetishiwa ‘ubuyu’ huo, Wikienda lilimtafuta mlimbwende huyo na kumfikishia madai hayo kisha kumweleza mabadiliko wanayotaka mashabiki na watu wake wa karibu ambapo alikuwa na haya ya kusema:

 “Siku zote ninavyojua mimi mapenzi hayachagui, suala la kumpenda nani kwa maana ya staa, kiongozi, fukara, mwenye elimu au asiyekuwa nayo na wengineo ni matakwa ya moyo wangu kutokana na ulipodondokea.
“Kama ni ishu ya kuwa bungeni ni suala la muda, wakati ukiwadia basi kila kitu kitakuwa sawa. Kama ni mchumba wasubiri watamuona siku ya ndoa lakini hao wengine wala sijatoka nao!”

KABLA YA DIAMOND, KIBA
Ukiachilia mbali Diamond na Kiba, pia Jokate aliwahi kukiri na kuripotiwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Mbongo anayekipiga kwenye Ligi ya Kikapu ya Marekani, NBA, Hasheem Thabeet.
Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. From my point of view is it is damn hard for an emancipated woman to get married now days maybe one out ten emancipated women will get married 'coz most of them they've what we call"ego&no respect to a man 'coz they think financial they've achieved something so they get this Iam above or equal to a men mentality" which's not fair so many of them ending up having children with different men or geting screwed every now and then by different men and at last when they are no more shinning like they used to be you find such women all alone without a partner damn sad

    ReplyDelete
  2. Awe bunge la wapi? hajatulia!!!!!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad