Rose Ndauka Atoa Siri ya Mambo Yake Kumnyookea

MKALI wa filamu Bongo, Rose Ndauka ametoa siri ya mambo yake kumnyookea kuwa imetokana na kumuhusisha Mungu kwa kila anachokifanya na wala si vinginevyo kama watu wanavyodhania.

Akizungumza na Amani, Rose ambaye kwa sasa anamiliki kampuni inayojishughulisha na kutengeneza Jarida la Rozzie, alisema kuwa Mungu ndiye aliyemtendea miujiza hiyo kwani asingemshirikisha asingekuwa hapo alipo.

“Siri kubwa ya mafanikio niliyonayo ni kumtegemea Mungu na hakuna namna yoyote kinyume na hapo niliyofanya. Kuna faida kubwa sana katika maisha yangu, nimeona na nimeshuhudia kabisa, wala sitathubutu kumuacha kamwe,” alisema Rose.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad