Sakata la Wema Sepetu na Petit Man Kutoelewana..Msanii Mirror Amkana Petit Man Laivu

Baada ya kuenea kwa tetesi kuwa kuna kutoelewana kati ya Petiti Man na Wema Sepetu,bado kumezidi kuwepo na kizungumkuti juu ya yupi msimamizi wa msanii Mirror ambae yupo chini ya Endles Fame.

Wakizungumza na Enewz kwa nyakati tofauti Petiti alisema kuwa yeye bado ni Manager wa msanii huyo lakini Mirror akikana kuendelea kusimamiwa na Manager huyo huku tukiona katika akaunti yake ya instagram amebadili jina la Mirror na kuweka wasanii wengine.

Kwa upande wa Mirror ameiambia Enewz kuwa Petiti anakusanya pesa kwa wadau kwaajili ya kazi zake lakini hafanyi kazi badala yake anatumia kwa matumizi yake binafsi huku akiongeza kuwa kisa kikubwa cha kutosimamiwa na yeye ni baada ya kumuona akijishughulisha na wasanii wengine.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad