Timu za Tanga Zaipa Mkono wa Kwaheri Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania

Klabu ya African Sports imeungana na vilabu vingine vya Tanga (Coastal Union na Mgambo JKT) kuipa mkono wa kwaheri ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara baada ya kuchapwa bao 2-0 na Mtibwa Sugar kwenye mchezo wa mwisho wa ligi uliochezwa kwenye uwanja wa Manungu Complex, Turiani, Morogoro.

African Sports na Mgambo JKT zote zilikuwa zikihitaji ushindi kwenye mechi zao za leo huku zikiombea mabaya timu za Ruvu JKT na Kagera Sugar ili zenyewe ziwe na uhakika wa kusalia VPL.

Lakini mabo yalikuwa tofauti baada ya Ruvu JKT kuichapa Simba kwenye uwanja wa taifa huku Kagera Sugar wakipata sare ya kufungana bao 2-2 dhidi ya Mwadui FC.

Kwenye uwanja wa Azam Complex, Mgambo imeshuka daraja kwa kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Azam FC. Mgambo iliyokuwa ikihitaji ushindi kwenye mchezo wa leo imejikuta ikishindwa kupata ushindi kwa mara nyingine mbele ya Azam ambao sare hiyo imewafanya wamalize kwenye nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Yanga.

Simba waliokuwa wakiwania nafasi ya pili wamechapwa na Ruvu JKT na timu hiyo iliyo chini ya kocha wa zamani wa Simba King Kibadeni imenusurika kushuka daraja.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad