Ulikuwa unafuatilia majaribio ya mtanzania Farid Hispania? C.E.O wa Azam FC ana taarifa hii

Baada ya kurejea kwa Farid Musa kutokea Hispania alipokuwa anafanya majaribio katika klabu ya Deportive Tenerife ya Ligi daraja la kwanza Hispania (Segunda), kila mtanzania anatamani kujua nini kinaendelea kwa staa huyo wa Azam FC na Taifa Stars.

Mwanzoni taarifa zilisikika kuwa kafaulu majaribio lakini mazungumzo kati ya Azam FC na Tenerife hayajafikiwa C.E.O wa Azam FC Saad Kawemba katoa taarifa rasmi

“Ni kweli Farid amefuzu na kuna makubaliano tunafikia kwa ajili ya maslahi ya mchezaji, kwanza wanapaswa wampe muda sio akishindwa kufanya vizuri mechi moja wamuache hapana wanapaswa wampe muda”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad