Faiza Ally: Natamani Kuhongwa, Kwa Sababu Sijawahi Kuhongwa Hata Siku Moja

Muigizaji na mrembo mwenye vituko kibao, Faiza Ally, amesema atafurahi sana endapo atampata mtu wa kumuhonga kwa sababu hajawahi kuhongwa hata siku moja.

Akizungumza kupitia kipindi cha Kubamba cha Times Fm, Bi dada huyo mwenye mtoto mmoja amedai ameanzia mbali kutafuta fedha na karibu kila kitu chake anajihudumia mwenyewe.

Natamani nipate mtu wa kunihonga, coz mimi kila kitu najifanyia mwenyewe, hata biashara yangu nmeisimamisha mwenyewe nilishawahi hata kuuza mama ntilie” Alisema.

Katika hatua nyingine muigizaji huyo ambaye anategemea kuiingiza sokoni filamu yake mpya muda si mrefu, ameweka wazi kuwa amenunua gari ya ndoto yake aina ya Landrover.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad