Marafiki wa Isaac, Aliyekuhumiwa Kwa Kumtukana Rais, Wamchangia Mil 4.5 ya Faini

Marafiki wa Isaac Habakuk pamoja na wadau ambao hawakupendezwa na hukumu dhidi yake ya kwenda gerezani miaka 3 au kulipa faini ya milioni 7 kwa kudaiwa kumtukana Rais Magufuli kupitia mtandao wa Facebook kwa kutumia neno bwege wamemkabidhi jumla ya shilingi milioni 4.5 kwa ajili ya kulipa faini kuepuka kifungo gerezani.

Akikabidhi fedha hizo Jijini Arusha mchana wa leo, mwakilishi wa marafiki hao, Ndg Ephata Nanyaro amesema fedha hizo zimekusanywa kutoka kwa marafiki mbalimbali ambao wametafutana kwa njia ya simu na kila mmoja kuchangia kuanzia sh 500 na kuendelea mpaka zikafika kiasi hicho.

Fedha hizo ni makusanyo ya michango ya makundi mawili, moja likiratibiwa na Ephata Nanyaro na lingine likiratibiwa na Malisa Godilistern, wote wanachama wa Chadema na ambao hutumia mitandao ya kijamii kueleza mawazo yao kuhusu mambo mbalimbali.

Nanyaro amesema wameamua kufanya harambee ya kumchangia kijana mwenzao aepukane na dhahama ya kutotumikia kifungo kwasababu kwa jinsi sheria ya makosa ya mtandao ilivyo, kila mwananchi yuko hatarini kupelekwa gerezani kwa sheria hiyo kwasababu inavifungu ambavyo vinakiuka msingi mkuu na uhuru wa binadamu kuwaza na kujieleza.

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mmemchangia lakini mmeharibu, kwani ilikuwa na ulazima gani kutangaza? si mngetoa kimya kimya

    ReplyDelete
    Replies
    1. Funga bakuri lako
      Inakuhusu nini ngedere wewe
      Usojuwa hata kuchamba

      Delete

Top Post Ad

Below Post Ad