Mtoto Mdogo wa Miaka 3 Abakwa na Baba yake Mzazi

Jeshi la polisi wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga linamshikiria mtu moja Ngasa Sakwa mwenye umri wa miaka 23 mkazi wa kitongoji cha lukelege, kijiji cha Masagala, kata ya Maganzo, wilayani humo, kwa tuhuma za kumbaka mwanae wa kike, Shida Ngasa, mwenye umri wa miaka 3, na kumsababishia maumivu makali, tukio hilo lilitokea juni 9, mwaka huu katika mji mdogo wa Maganzo wilayani humo.

Kesi hiyo yenye namba MGZ/IR/256 imefunguliwa katika kituo kidogo cha polisi Maganzo na bibi wa mtoto huyo, Milembe Luhende wa kijiji hicho kufuatia kubaini mjukuu wake kufanyia kitendo hicho cha kikatili na mwanae wa kiume ambapo siku ya tukio kijana huyo, anayefanya kazi ya ulinzi katika nyumba ya kulala wageni ya Nsamaka iliyopo Maganzo  alimchukua mtoto huyo na kwenda naye kazini kwake ambapo baada ya kumrejesha nyumbani ndipo walipogundua kufanyiwa kitendo hicho.

Kitendo hicho kinahusishwa na imani za kishirikina na matumizi ya dawa za kulenywa kutokana na uhalisia wa eneo la maganzo wakazi wake kujihusisha shughuli za uchimbaji madini huku serikali ikisisitiza mhusika achukuliwe hatua kali za kisheria.
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Atiwe jiti la mkundu Na yeye jinga hilo

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad