Quick Racka Afunguka Haya Kuhusu Yeye na Kajala


Mkali wa Bongo fleva Quick Racka amefunguka juu ya uhusiano wake na msanii wa Bongo muvi Kajala Masanja.

Akizungumza na Enewz Quick Racka alisema kuwa yeye na bongo muvi star huyo ni washikaji wa karibu sana na urafiki wao una miaka miwili sasa, huku kila mtu akiwa na kazi zake.

“Tunashauriana yaani kama washikaji na nampenda kama mshikaji wangu kama hamuelewi hata picha hamuoni”,alisema Quick Racka huku akiongezea kuwa kwasasa studio yao ya switch inafanya kazi ya kumsimamisha producer wao Rufe ajulikane ndipo watakaporudi kujihusisha na msanii mmoja mmoja”, alisema Quick Rocka.

Rapper Quick Rocka ambaye kwa sasa anafanya kazi na Switch Records, pia ameelezea mipango yake ya kufanya muziki wa aina tofauti tofuti, huku tetesi zikisema sasa anataka kufanya muziki wa bolingo

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Bonge la aibu hilo Kajala wewe ulimtangaza huyo kama mpenzi wako lakini mwenzio anakukuna kwenye social media anasema mko watu wa karibu tu lakini si wapenzi, ngoja nicheke, he he

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad