Spika Job Ndugai Anaendelea vyema Nchini India....

Naibu Spika wa Bunge Tulia Ackson amesema kwamba watanzania wasikubali uvumi unaoenezwa na baadhi ya mitandao kwamba Spika wa Bunge Job Ndugai hali yake ni mbaya bali waamini kwamba hali ya Spika ni njema na anaendelea vizuri na matibabu.

Naibu Spika ameyasema hayo baada ya kumalizika kusomwa kwa bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016 & 2017 na kusisitiza kwamba Naibu Spika ni mzima na anawatakia watanzania mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani.
''Kumekuwa na uzushi mkubwa kuhusu afya yake, ni kweli alikwenda India kwa ajili ya kupata matibabu kama alivyoambiwa na daktari wake alipotoka huko mwaka jana'' amesema Naibu Spika Tulia.
Aidha Naibu Spika amesisitiza kwamba Spika wa Bunge bado anaendelea kuwasiliana na viongozi wa serikali pamoja na baadhi ya wananchi wa jimbo lake.
Hata hivyo Naibu Spika amewataka wananchi kuendelea kumuombea ili aweze kurejea salama kuendelea na kazi zake kama kawaida.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mungu atakupa afya urudi salama salimini, Ulitumikie taifa.

    ReplyDelete
  2. Get well Soon Job Ndugai, The Speaker of Tanzania Parliament

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad