Watatu Wafa Wakidaiwa Kula Mihogo yenye Sumu

Watu watatu wamefariki dunia baada ya kula mihogo inayodhaniwa kuwa na sumu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amesema jana kuwa tukio hilo juzi saa tisa mchana katika Kijiji cha Kauzeni, Manispaa ya Morogoro.

Amesema watu hao ni kati ya watano waliokula mihogo hiyo, lakini wawili walinusurika baada ya kuwahishwa Hospitali ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Mzinga kwa matibabu.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad