Wolper Adai Kiingereza Kilimfanya Adanganyike Kwenda South Africa na Mkongo

Wolper na Aliyekuwa mchumba Wake 
Msanii wa filamu bongo, Jacqueline Wolper amesema alijikuta akidanganyika kwenda Afrika Kusini kwasababu alitaka akasomee Kiingereza, lugha anayoamini ni muhimu wake.

Akiongea kwenye kipindi cha Take One, kinachoruka kupitia Clouds TV, Wolper amesema kuwa chuki zilizopo kwenye kiwanda cha filamu na tatizo la kutoijua lugha hiyo ndiyo sababu nyingine iliyomfanya akubali kumfuata mpenzi wake Mkongo Afrika Kusini.

“Ndiyo maana mimi mwenzangu nilikubali kudanganyika kwenda South Afrika kusoma kizungu,” alisema.

“Mimi mchaga napenda hela, ilikuwa siyo rahisi kukubali kwenda kusoma Afrika Kusini na kuacha sanaa yangu napata mwenyewe milioni nne au tano maisha yangu yanaenda. Lakini nimekubali kwenda kule kusoma lugha at least nivuke hatua niende sehemu nyingine kwa sababu wenzetu huku wana chuki na hakuna kitu kinachoendelea vitu vimefeli. Lakini vitu vikagoma, I am sure kwamba bado sijachelewa nitafanya, nitajitahidi nitafika kule ninapotaka kufika,” alisema Wolper.

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hili lizee nalo tumelichokaaaaaa

    ReplyDelete
  2. anakumbuka shuka asubuhi. aibu hana jipya kabikia kumbemenda watoto.

    ReplyDelete
  3. endelea kutapatapa utaongea hili utarukia lile mkongo ametulia tuli ye alitaka nyapu alishaipata kiulaini basi... kasepa kwa mkewe kakuachia doa na mirembe amekutua. utabaki na udungaembe wako!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad