Bella Asema Hana Tatizo na Luteni Kalama Baada ya Kufunga ndoa na Rafiki yake, Amnanga Rafiki yake

MISS Ruvuma 2006 Isabellah Mpanda ‘Bella’ amesema hajapenda kitendo alichofanya rafiki yake wa karibu cha kufunga ndoa na aliyekuwa mpenzi wake, Luteni Kalama.

Akiongea na Bongo Yetu  Jumanne hii, Bella amesema yeye hana tatizo na Kalama kwa kuwa ni watu ambao wanafanya kazi pamoja.
“Mimi kama mimi huyo msichana hana akili, pia ni ushamba nafikiri,” alisema Bella. “ Sababu kuna raha gani kufunga ndoa na shemeji yako. Alafu hakuna kitu kibaya kama kujiozesha kwa mume, kila kitu unafanya wewe alafu mwanaume hakupendi, unaishi vipi?,”

Aliongeza, “Lakini mimi na Kalama nashukuru mungu tupo vizuri sana, Kalama ni rafiki yangu, kwa sababu tumetoka mbali sana na tunajuana, ni miaka 16 mpaka tunakuja kuachana, kwa hiyo sina tatizo na Kalama na nitaendelea naye kufanya kazi. Lakini mimi huyo mwanamke simpendi kabisa kutoka moyoni mwangu kwa sababu sijamkataza mimi Kalama kuoa, lakini angeoa mwanamke mwingine lakini siye huyo mwanamke ambaye alikuwa rafiki yangu, tunakula pamoja, tunalala pamoja, kwa hiyo ni kitu chakuchekesha sana, lakini nimekuja kugundua ni ushamba wa mwanamke, anataka nayeye atembee na supastaa labda na yeye atakuwa supataa, unakuwaje supastaa meno yenyewe yameoza, mwanamke una sura mbovu, mimi ni mtoto mkali, mtoto miss nisiyechuja,”

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mbona povuuuuuu... bibie m2anaume si ulimiacha mwenyewe au...we mwenyewe huna sura ya kivutia hata yani ww na huyo bint huyo bint ni mara elfu10 mzuri zaidi yako

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad