Hakuna Ubaya Mimi Kutoka Kimapenzi na Kajala- Msami

Msanii Msami ambaye kwa sasa anafanya poa na wimbo wake wa ‘Mabawa’ amefunguka na kusema kuwa yeye ni mwanaume na Kajala ni mwanamke hivyo kwa kile ambacho kinazungumzwa na watu kuwa huenda anatoka naye kimapenzi

‘Si jambo baya kwani Kajala ni mtoto wa kike na yeye ni mwanaume hivyo chochote kinaweza kutokea kati yao’.

Msami alisema hayo kupitia kipindi cha eNEWS na kudai kuwa maneno yanazungumzwa juu yake na Kajala huenda yapo na kama hayapo labda yanaweza kuja kutokea, ila anadai yeye na Kajala ni washikaji, ambao wamekuwa wakishirikiana na kusaidia mambo mengi.

“Unajua Kajala ni mtu wangu wa karibu sana, tunaongea mengi na kushauriana vingi japo ukaribu wetu umetafsiriwa tofauti na baadhi ya watu wakidhani tunatoka kimapenzi, japo si vibaya kwani sioni kama kuna ubaya mimi kutoka na Kajala. Sijasema nina mahusiano na Kajala ila ikitokea tukawa wapenzi tunaweza kuzungumza mimi na yeye kujua hatma yake na mume wake ambaye anatumikia kifungo kwa sasa” alisema Msami

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad