Hii Hapa Kauli ya Mbowe Kuhusu BAVICHA Kwenda Kuzuia Mkutano wa CCM...Awataka Kusitisha Zoezi

Baada ya baraza la vijana wa CHADEMA ‘BAVICHA’ kuwa na mkakati kuzuia mkutano mkuu wa CCM uliopangwa kufanyika Dodoma kwa kuandaa vijana 5000 kutoka sehemu mbalimbali nchini kwenda kuzuia mkutano huo utakaotumika kumkabidhi Rais Magufuli uenyekiti wa CCM.

Leo July 10 2016 Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amezungumza na waandishishi wa habari Arusha na kuwataka vijana hao kusitisha zoezi hilo hadi hapo chama kitakapotoa tamko……..

’Mimi nawataka vijana wa mikoa yote wa CHADEMA waache CCM wakaendelee na mikutano yao, hatuna hofu na mkutano wowote wa CCM ila tunalitaka jeshi la polisi lijue kwamba hauwezi ukaongoza Taifa na kutenda haki ukiwa na double Standard’

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mbowe!! Wewe wakuwakumbusha jjeshi letu la Polisi?? Hivyo maana ya dabo standadi Ni nini??

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad